Jumanne 10 Juni 2025 - 21:49
Kama utawala wa Kizayuni utafanya kosa lolote lile, basi wafahamu kwamba, Vinu vilivyo fichwa vya Nyuklia vya Utawala huo vipo kwenye lengo la vikosi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

Hawza/ Baraza Kuu la Usalama wa Taifa limetoa taarifa kufuatia operesheni tata za kijasusi za askari wa Imam Zaman kwa kusema: Endapo utawala wa Kizayuni utafanya tukio lolote la mashambulizi, basi ufahamu kwamba, vituo vya nyuklia vilivyo ficha vya utawala huo vipo katika orodha ya malengo ya vikosi vya Jamhuri ya Kiislamu na vitashambuliwa mara moja.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, kutoka Tehran, sehemu ya taarifa ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa imesema: Huu ni ushindi na mafanikio makubwa ya kijasusi, sehemu muhimu ya mipango ya busara na hatua za kimya kimya zisizo na kelele za mfumo mtakatifu wa Kiislamu dhidi ya fujo za maadui, ambayo sehemu nyingine muhimu ni juhudi zinazofanywa usiku na mchana na vikosi vya ulinzi katika kuunda uwezo wa operesheni unaolingana na udhaifu na nguvu za utawala wa haramu wa Kizayuni na wanao wakingiabkifua.

Leo hii upatikanaji wa taarifa hizi na kukamilisha mzunguko wa operesheni hii, umewezesha wapiganaji wa Kiislamu kushughulikia mara moja shambulio lolote la utawala wa Kizayuni dhidi ya vituo vya nyuklia vya taifa kwa kushambulia vituo vyake vya nyuklia vilivyo fichwa na kuwapiga hatua kwa hatua dhidi ya vitisho vyovyote vinavyohusiana na miundombinu ya kiuchumi na kijeshi, kulingana na aina ya shambulio.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha